Monday, June 28, 2010

REDDS MISS KINONDONI KIBOKO YAO


Hii ndiyo tano bora ya shindano la kipaji la Redds Miss Kinondoni lililofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye Hoteli ya Giraffe Ocean View iliyoko Mbezi jijini Dar es salaam warembo wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya jaji mkuu Gerald Hando kutangaza matokeo, kutoka kulia ni Irene Hezron, Salma Ally, Alice Lushiku, Caroline Mbembo na Tamara Ally.

Hapa majaji wakiwa makini ili kuhakikisha kazi yao inakwenda vizuri katika shindano hilo.
Huyu yeye alichora bango lenye ujumbe wa kupambana na ugonjwa wa ukimwi kama bango lake linavysomeka.

Huyu alitangaza lakini anelekea yuko sawasawa na kama kuna redio inahitaji mtangazaji hebu jaribuni kuongea na huyu anaweza kuwafaa.
Huyu akalimwaga sebene la kukata na shoka.
Huyu naye akacheza nyimbo ya Kiarabu.
Shindano la kipaji lilianza kwa mrembo huyu kucheza.

No comments:

Post a Comment